Tuesday, September 1, 2015

Dr. Slaa, Haya ndiyo aliyoyasema kuhusu Lowasa, CHADEMA na msimamo wake kisiasa

Dr. Slaa Dr Slaa katika hoteli ya Serena akiwa na walinzi wake 7, amefika na kuamua kuweka kila kitu wazi kuhusu ukimya wake. Soma hapo chini alichozungumza
Slaa: Kila mtu ana kiu ya kusikia Dr Slaa anasema nini, sijawahi kuona waandishi wengi hivi
Slaa: Wengi mnafahamu sina tabia ya kuyumbishwa, ninasimami a lile ninaloamini, ijulikane kama binadamu sina chuki na mtu
Slaa: Mimi sikuwa likizo kama mlivyoambiwa na wengine. Nimeamua kuachana na siasa tarehe 28 Julai 2015 saa 3 usiku.
Naomba ijulikane kuwa nilishiriki majadiliano ya awali juu ya ujio wa Lowassa ndani ya CHADEMA, ila sikuafiki ujio wake.
Slaa: Mchakato ndani ya CHADEMA ulianza mapema na jina langu lilipitishwa lakini bado sikuitangaza popote.
Slaa: Suala la Msingi ni kuangalia kama ni ASSET au LIABILITY, ASSET kwa maana kwamba anakuja na watu wangapi kwenye chama
Slaa: Tuliambia anakuja na wabunge wanaomaliza muda wao zaidi ya 50 na viongozi wengine toka CCM.
Slaa: Siku zikapita sikupewa majina ya wabunge hao, wenyeviti wa CCM mikoa wala makatibu wakuu.
Slaa: Upotoshwaji kwamba Dr Slaa alikubali toka mwanzo si kweli naomba viongozi wangu waseme kweli.
Slaa: Kamati kuu tumekaa toka saa 9 hadi 12:30 kikao kikavunjika, ikasemwa iundwe kamati ndogo kunishawishi, nikakataa.
Slaa: Niliandika barua ya kujizuru ndani ya kamati kuu kwa mwenyekiti wakati huo akiwa Profesa Safari, ambaye aliichana.
Slaa: Mimi mwanasiasa niliyozoea naamini siasa ni sayansi haitaki uongo, haitaki udanganyifu.
Slaa: Maamuzi yaliyofanywa, yalifanywa na mimi kwa ridhaa yangu mwenyewe.
Slaa: Sisi katika familia yetu tumezoea propaganda hizo, nishasema kama mna ushahidi muulete
Slaa: Nataka niwahakikishie D. Slaa na watoto wake wameendelea kula mihogo kama tulivyoahidi maana pesa imesaidia watanzania
Slaa:Ni lazima mwanasiasa yoyote duniani hataji jina linachafuliwe, hata Dr Slaa hataki jina lake lichafuliwe ni haki yangu.
Slaa: Jambo ambalo nataka nifafanue ni suala zima la LIABILITY au ASSET, ASSET nimelieleza, wamekuwa waongo hawakutekeleza
Slaa: Mtu ambaye hata mwezi mmoja haujapita tangu useme CCM ikimteua Lowassa atajitoa, leo anasema ni msafi.
Slaa: Wenyeviti waliokuja CHADEMA wote toka CCM ni mzigo, makapi.
Slaa: CHADEMA inachukua mtu kwa sifa ya wizi wa kura, kama hatutaki kuiba kura sisi tunaenda kufanya
Slaa: Suala la ASSET sikupata majibu, ndio maana hadi leo viongozi wangu wamepata kigugumizi, naongelea kwanini nimeondoka.
Slaa: Mimi padri , yaani nikubali kuweka mkataba na shetani kwaajili ya kuiondoa CCM? unaondoa CCM kwa ‘progamu series
Slaa: Watu waliikubali CHADEMA kwaajili ya misingi ya uadilifu, leo tuna unadilifu?
Slaa: Duniani kote tuhuma zinatolewa na ni jukumu la serikali kutoa majibu. Kama watu hawajui siasa bora wakae kimya.
Slaa: CCM siwezi kuwahurumia, hata Lowassa hapa alipofika ni kwakuwa CCM ilimlea.
Slaa: Kama ukikuta choo cha kitanzania, ukapakua kilichoko ndani ya choo na kuweka chumbani kwako, ipi ni choo?
Slaa: Mimi nilikuwepo 2008 wakati tunajadili RICHMOND tunapozungumza masuala hayo ni kwakuwa tunayajua na tuliyaishi Bungeni
Slaa: Lowassa tunamtuhumu mengi , mimi simtuhumu kwa RICHMOND tu, 2010 mimi nilimwambia atumbie hadharani RICHMOND ya nani
Slaa: Ni afadhali nipotee kwenye siasa Tanzania na duniani kote kuliko kuyumbishwa na misimamo yangu.
Slaa: Mimi nimeletewa rushwa asubuhi, nikamuuliza aliyeleta kama mimi unanipa milioni 500 unazo ngapi?
Slaa: Mwanzo wa RICHMOND lazima urudi kwanza kwenye taarifa ya baraza la mawaziri februari, 2006.
Slaa: Naomba mtambue kwamba suala hili la RICHMOND halikuanzia kwa Kikwete bali lilianzia kwa Mkapa.
Slaa: 2006 feb 10, Waziri mkuu alikuwa Lowassa, sasa leo unapokuja kunambia hakuhusika maanake nini?
Slaa: Ripoti ya Mwakyembe alitoa option mbili, Waziri Mkuu ajipime au Bunge lijadili na kutoa uamuzi, akakimbilia kujiuzulu.
Slaa: Lowassa dakika ya mwisho aliingilia, hakusaini yeye ila aliagiza personal assistance wake akasaini.
Slaa: Watu wanauliza kwanini namsema Lowassa mwenyewe ni kwakuwa anagombea urais wa nchi.
Slaa: Nendeni basi Monduli kwa Lowassa na Karatu mlinganishe wakati nikiwa mbunge, halafu tuone huyu mnayemuita mtendaji.
Slaa: Mnasema habari za shule ya kata, hizi sio zao lake ni upotoshwaji, aseme alibuni wapi wazo hili.
Slaa: Ugomvi wangu na Masha ni kwasababu nilitoka hadharani na kusema Masha umeingilia mchakato wa serikali, nikawa adui.
Slaa: Wakaandika uongo kuwa RICHMOND ni kampuni ya stationary wala sio umeme
Slaa: Waziri Mkuu anajua yote halafu ananyamaza, kama alikuwa hajui ni mzembe, kama ni mzembe hafai tena kuwa Rais wa nchi.
Slaa: Kumbuka Tanesco ni chombo kinachojitegemea, ikaagizwa kusaini mkataba ambao haikujadili, maanake ni nini?
Slaa: CHADEMA tumaini jipya lilijengekea, vijana wanaliamini ninaogopa, kwa masikitiko ninasema sitaki baadaye tufike pabaya
Slaa: Kama CHADEMA leo inafika hatua ya kujaza uwanjani watu kwa mabasi halafu mnasema kuna mafuriko,siko tayari kuwa zezeta
Slaa: Udanganyifu huu wa kujaza watu kwa kubebwa na magari kuja uwanjani wakajaza uwanja walikuwa nao CCM
Slaa: Nimewasikia CHADEMA jangwani, waliyoongea ni sehemu kubwa ya ilani ambayo ilishaandaliwa zamani, hakuna kipya.
Slaa: Kinachoniumiza ni sisi kuwa wabovu zaidi ya CCM.
Slaa: Nataka Lowassa ajue kuwa tunajua, Scotland inatuandikia kuwa achunguzwe kwa paundi milioni 400 alizopeleka marekani.
Slaa: Halafu wanasema nikizungumza eti nitaharibu sifa yangu, wacha iharibike.
Slaa: Mimi nimefundishwa kukemea maovu.
Slaa: Leo anakuja mtu hapa anatuambia nyamazeni? Mimi sitaki kuingia kwenye mambo ya akina babu seya.
Slaa: Leo baadhi ya vyuo vinatumia kesi ya babu seya kufundishia kama kesi ya ulawiti halafu lowaasa anasema ataifuta
Slaa: Nani aliyeagiza maaskari waingie na mbwa pale mwembe chai msikitini? Sumaye huyu huyu aliagiza.
Slaa: Lowassa akili yake ipimwe, kesi ya ulawiti Rais hapaswi kuingilia, anaingilia uhuru wa mahakama
Slaa: Ni afadhali kutokuwa na Rais wa aina hii, Rais ambaye anatumia udanganyifu kwakuwa watu hawajasoma hafai.
Slaa: Waswahili wanasema ukiumwa na nyoka basi hata jani ulikimbie, inabidi tuhakikishe kwamba tunakuwa makini
Slaa: Alipokuwa Waziri Mkuu haya matatizo yanayotokea leo hayakutokea?
laa: Mtu aliyesababisha migogoro ya mipaka halafu leo anataka kuwa Rais?
Slaa: Wapo watakaosema ameichana CHADEMA, ameijenga CCM. Ukweli haugawanyiki, kama yameitandika CHADEMA ndio ukweli ulivyo
Slaa: Nimesema sina chama ila mimi ni mtanzania, nitawatumikia watanzania kwa vipawa alivyonipa Mwenyezi Mungu.
Slaa: Nimeombwa kugombea urais kwenye vyama vitano ila nimekataa kwakuwa mimi siamini katika kuhama hama vyama.
Slaa: Mshenga niliyemtaja, alisema kanisa la kilutheri lote linamuunga mkono Lowassa, na maaskofu wa katoliki 30 wamehongwa
Slaa: Sitaenda chama chochote, nimesema sina chama, siasa kwa maana ya chama sina, ila siasa kwa ninayoamini.
Slaa: Sijaja kufanya kampeni leo, nimekuja kuwakumbusha Watanzania wasije wakajuta kama ambavyo tunajuta kwa kosa tulilofanya 2005 na 2010.

0 comments:

Post a Comment